Na Benson Rioba
KAJIADO, Kenya (Thomson Reuters Foundation) - Justus Opiyo anaishi katika chumba kimoja kilicho miongoni mwa nyumba zaidi ya hamsini zinazojengwa na paneli zilizotengezwa kutoka plastiki laini almarufu polystyrene katika kaunti ya Kajiado, Kusini mwa Kenya. Opiyo anasema kuwa chumba hicho kina manufaa kuliko vyumba vyote ambavyo amewahi kuiishi.
Chumba hicho huhifadhi joto hata wakati kiwango hicho kinapobadilika nje kinyume na nyumba nilizokuwa nikiishi hapo awali, opiyo asema. Aliongeza kuwa nyumba hiyo ilimkukinga kutokana na viwango vya juu vya joto vilivyoshuhudiwa mapema mwaka huu.
Ujenzi wa nyumba kwa kutumia polystyrene ni teknolojia mpya ya ujenzi ambayo imeanza kutia fora katika sekta ya ujenzi nchini Kenya. Paneli zinazotumiwa katika ujenzi huu zimetengezwa kwa plastiki nyepesi ambazo huzalishwa mafuta yanaposafishwa na huwa na asilimia 98 ya hewa.
Ili kujenga nyumba hizi za kisasa, polysterene huwekwa katikati ya nyaya mbili zenye matundu kisha kumwagiliwa simiti ili kuusimamisha wima na kuupa ukuta nguvu.
Kwa vile polysterene ina hewa, nyumba hizi huweza kudhibiti mabadoliko ya hali ya anga kuliko zile nyumba zilizotengezwa na mawe ama mbao. Hii ni kwa sababu hewa haina uwezo wa kupitisha joto hivyo nyumba hizo huwa joto wakati nje kuna baridi na husalia baridi wakati kuna joto nje.
Romanus Otieno, mhadhiri wa mipango ya miji katika chuo kikuu cha Nairobi anasema kuwa ingawa polystyrene inazalishwa kutoka kwa mafuta manufaa yake ni mengi hasa ikizingatiwa ujenzi huu unatumia maji kidogo sana. Anaongeza kuwa ujenzi huo utakuwa wa manufaa katika ujenzi wa nyumba katika miji na maeneo kame ambao kuna uhaba wa maji.
Kwa upande wake, Dennis Muli, ambaye ni msanifu wa majengo katika kampuni ya Gem Archplans jijini Nairobi anasema kuwa uepesi wa Polystyrene unafanya ujenzi wa nyumba kutumia miti michache hivyo kuzuia ukataji miti.
NYEPESI LAKINI DHABITI
Otieno ansema kuwa nyumba wastani zenye vyumba viwili vya kulala ambazo zimetengezwa na polystyrene hugharimu gharimu Dolla za Kimarekani 6,700, ilihali zile zilizotengezwa na mawe hugharimu maradufu ya kiwango hicho. Hali hii, anasema imechangiwa na idadi ndogo ya wajenzi wanaojenga nyumba za polystyrene kwani paneli hizo ni rahisi kubeba na kuwekeza hivyo mishahara inayolipwa wafanyikazi ni duni.
Aliongeza kuwa urahisi wa kujenga nyumba za polystyrene huenda ukachangia pakubwa katika kumaliza uhaba wa nyumba humu nchini.
Kilomita chache kutoka eneo la Kandisi ambapo Opiyo anaishi Kuna Orofa ya Polystyrene yenye vyumba 20 katika mtaa wa Ole Kasasi.
Hii ni baadhi ya miradi ya ujenzi wa kutumia Polystyrene ulioanzishwa nchini Kenya na makampuni tofauti zikiwemo orofa zilizojengwa katika jiji la Kisumu na kampuni ya Koto Corp kutoka Malaysia.
Lakini teknolojia hii mpya ya ujenzi bado ijaenziwa kikamilifu na kunavbaadhi ya wawekezaji, na wapangaji ambao wanatilia shauku udhabiti wa vyumba vya polystyrene.
Taib Ali, mjenzi katika orofa ya Ole Kasasi anasema kuwa wengi humkejeli kwa kuuliza ni lini orofa hiyo ya makaratasi itakapokamilika kwani watu huamini kuwa orofa hiyo ni hafifu kwani Polystyrene huvunjika kwa uraisi.
Mary Nkatha, ambaye anaishi katika chumba cha mawe karibu na orofa ya Ole Kasasi bado hajasawishiwa kikamilifu kuwa polystyrene inaweza kudhibiti uzito wa nyumba kwa muda mrefu na anahofu kuwa nyumba huenda ikaporomoka. Ansema kuwa atasuburi na kutazama udhabiti wa nyumba hizo kabla ya kufany uamuzi iwapo ataishi katika nyumba hizo.
Lakini Muli ambaye ni msanifu wa majengo anasema kuwa nyumba zailizotengezwa na polystyrene ni dhabiti kama zile zilizotengezwa na mawe bora tu utaratibu wa ujenzi ufwatwe kikamilifu.
Muli aliongeza kuwa ujenzi wa nyumba kutumia Polystyrene zimekuwa na mafanikio katika nchi ya Japan ambapo hutumiwa kujenga nyumba ndogo zenye umbo la kuba.
USALAMA KWANZA
Muli anazitaka serekali na mashirika yasio ya kiserekali kuwakatika mstari wa mbele kupigia debe ujenzi wa nyumba wa polystyrene kwani ni ya gharama ya chini na inakuza mazingira.
Aliongeza kuwa kuna haja ya utendakazi wa hali ya juu kwani teknolojia hii bado ni mpya ilikuzuia majanga kama kuporomoka kwa majengo kutokana na ujenzi mbaya mbali na kutafuta njia mwafaka ya kusaga uchafu unayotokana na polystyrene na kutumia upya.
Msemaji wa Koto, Hillary Wesonga alisema kuwa kampuni yake imeanzisha kitengo cha kusaga uchafu unaotokana na polystyrene, ingawa bado tatizo la uchafu halijakuwa kubwa nchini Kenya kwani teknolojia hii ni mpya. Hata hivyo, mambo huenda yakabadilika katika siku za usoni na kiwango cha uchafu kikaongezeka.
Otieno alihimiza bei za paneli za polystyrene kuteremushwa zaidi iwapo teknolojia hii mpya itaimarika na kutia fora nchini Kenya. Otieno alisema kuwa umuhimu wa ujenzi wa nyumba za bei ya chini ni kumaliza msongamano wa watu katika maeneo ya miji gharama ya juu ya nyumba itahujumu mradi huo.
Otieno aliongeza kuwa wajenzi wa nyumba wanapaswa kuzingatia miundo ambayo itasaidia kukuza mazingira kama kutengeza hifadhi za maji ya mvua na kunasa miale ya jua mbali na kuzingatia vipengee muhimu vya usalama na majanga yanayosababishwa na mabadiliko ya anga.
Mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu, jumba moja liliporomoka jijini Nairobi na kuuauwa watu wapatao 50 baada ya mvua kubwa kunyesha
Our Standards: The Thomson Reuters Trust Principles.