Na Isaiah Esipisu

MBEERE, Kenya (Thomson Reuters Foundation) – Wakulima katika maeneo kame za mashariki na kaskazini mwa Kenya wamegundua mbinu ya kuendelea kufanya biashara hata maji yanavyozidi kudidimia, kwani sasa wanafuga samaki aina ya kambale.

Sylvester Kinyori asema kuwa hiki ndicho chanzo cha mapato yake siku hizi. Bwana huyo mwenye miaka 32 anaendesha kioski katika mji wa Isiolo ambapo anauza bidhaa za samaki kutoka kwa wakulima wa eneo hilo ambao wamegeukia ufugaji samaki.

Kinyori, ambaye ni mzaliwa wa Turkana, eneo la wafugaji kaskazini mashariki mwa Kenya, sasa anaendesha maisha kwa kuuza minofu ya samaki zilizopikwa pamoja na mayai, na mikate.

Wakulima wadogowadogo walianza kufuga samaki katika maeneo haya miaka nne zilizopita, baada ya shirika moja la kibinadamu kuwaonyesha njia rahisi ya kutega maji ya mvua katika mabwawa ya kinyumbani.

Maji hayo huwekwa katika mabwawa yaliyochimbwa katika boma, na yameundwa kwa kutumia karatasi la plastiki nzito ili kuzuia maji kumezwa na mchanga.

Mbinu hii ilianzishwa na wenyeji wa Yatta mashariki mwa Kenya ambao walijumuika pamoja ili kutafuta mbinu za kuepuka kutegemea misaada, ijulikanayo kama Mwolio, katika lugha ya Kikamba.

Baada ya mafanikio ya kutema misaada mnamo mwaka wa 2009, shirika la ActionAid Kenya liliamua kueneza mbinu hizo kwa wakaazi wengine kote mashariki na kaskazini mashariki mwa Kenya.

Sehemu hizo ni kame, ambapo wakati mwingine hupokea mvua iliyo chini ya milimita 150. Sehemu hizo zina mito za msimu, nyinginezo ambazo hufurika kwa masaa machache tu, baada ya mvua kubwa, huku ikiwalazimisha akina mama kuchimba visima katikakati mwa mito ili kutega maji yaliyonaswa chini ya mchanga.

Topics
fod-env Adapting to Climate Change fod-env fod-rig