TANDALE, Tanzania, Januari 4 (Thomson Reuters Foundation) —Taswira ya ndege ndogo isiyo na rubani inayoelea angani kwenye mitaa ya Tandale kutathmini eneo lenye watu wengi linaloathiriwa na mafuriko mara kwa mara ilizua taharuki miongoni mwa wakazi wa eneo hilo waliochoshwa kabisa na mafuriko ya mara kwa mara.

“Ninafurahi kuona kwamba hatua zinachukuliwa kudhibiti mafuriko, alisema Happy Malimbo, mkazi wa eneo hilo mwenye umri wa miaka 35.

Kwa kusaidiwa na ndege hizo zisizo na rubani, mamlaka za jiji wanaandaa mpango kulinda na kusaidia wakaazi wa maeneo yanayoathiriwa na mafuriko, kama vile Tandale, na kutoa mwanya wa matumaini kwa wakaazi hao.

Tangu mwaka 2013, halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekuwa ikishirikiana na Benki ya dunia na wadau wengine, wakiwemo Shirika la Msalaba Mwekundu, na shirikisho la Open Geospatial kupima barabara, mifereji na madimbwi ya maji ya mafuriko kutumia ndege zisizo na rubani.

Ukiitwa Ramani Huria, mradi huo unalenga kusaidia jamii kwenye maeneo ya msongamano kutengeneza ramani sahihi za maeneo yao, ambazo zaweza kutumika kupunguza hatari ya mafuriko na kusaidia jitihada za uokozi, maofisa wa jiji wamesema.

Mafuriko huja kila mwaka Tandale, moja ya maeneo yenye makaazi holela jijini Dar, hata hivyo ukosefu wa mikakati ya kukinga mafuriko ina maana kwamba mafuriko ya asili husababisha janga kuu.

Wenyeji wanasema wamekuwa wakipata hasara kila mara kutokana na mafuriko, yanayowaacha mamia bila ya makazi.

“Nilipoteza mali yangu nyingi, nyumba yangu ilivyozingirwa na mafuriko mwezi Aprili mwaka jana,” alisema Malimbo, Mwenye watoto watatu.

Ikiwa zaidi ya asilimia 70 ya wakazi wake wakiishi kwenye makazi holela, Dar es Salaam, jiji kubwa nchini Tanzania liko katika hatari kubwa ya mafuriko, hasa kwenye maeneo ya msongamano kama Tandale.

Mvua kubwa hunyesha mara mbili kila mwaka, mara nyingi  ikisababisha mafuriko makubwa yanayowalazimu maelfu ya watu wahame nyumba zao na kusababisha hasara ya maelfu ya dola za marekani.

Topics
Extreme Weather hum-nat